6 Ee BWANA, uyasikie maombi yangu;Uisikilize sauti ya dua zangu.
7 Siku ya mateso yangu nitakuita,Kwa maana utaniitikia.
8 Katikati ya miungu hakuna kama Wewe, Bwana,Wala matendo mfano wa matendo yako.
9 Mataifa yote uliowafanya watakuja;Watakusujudia Wewe, Bwana,Watalitukuza jina lako;
10 Kwa kuwa ndiwe uliye mkuu,Wewe ndiwe mfanya miujiza,Ndiwe Mungu peke yako.
11 Ee BWANA, unifundishe njia yako;Nitakwenda katika kweli yako;Moyo wangu na ufurahi kulicha jina lako;
12 Nitakusifu Wewe, Bwana, Mungu wangu,Kwa moyo wangu wote,Nitalitukuza jina lako milele.