3 Maana nafsi yangu imeshiba taabu,Na uhai wangu umekaribia kuzimu.
4 Nimehesabiwa pamoja nao washukao shimoni;Nimekuwa kama mtu asiye na msaada.
5 Miongoni mwao waliokufa nimetupwa,Kama waliouawa walalao makaburini.Hao ambao Wewe huwakumbuki tena,Wametengwa mbali na mkono wako.
6 Mimi umenilaza katika shimo la chini,Katika mahali penye giza vilindini.
7 Ghadhabu yako imenilemea,Umenitesa kwa mawimbi yako yote.
8 Wanijuao umewatenga nami;Umenifanya kuwa chukizo kwao;Nimefungwa wala siwezi kutoka.
9 Jicho langu limefifia kwa ajili ya matesoBWANA, nimekuita kila siku;Nimekunyoshea Wewe mikono yangu.