20 Nimemwona Daudi, mtumishi wangu,Nimempaka mafuta yangu matakatifu.
21 Ambaye mkono wangu utakuwa thabiti kwake,Na mkono wangu utamtia nguvu.
22 Adui hatamwonea,Wala mwana wa uovu hatamtesa.
23 Bali nitawaponda watesi wake mbele yake,Nitawapiga wanaomchukia.
24 Uaminifu wangu na fadhili zangu atakuwa nazo,Na kwa jina langu pembe yake itatukuka.
25 Nitaweka mkono wake juu ya bahari,Na mkono wake wa kuume juu ya mito.
26 Yeye ataniita, Wewe baba yangu,Mungu wangu na mwamba wa wokovu wangu.