26 Yeye ataniita, Wewe baba yangu,Mungu wangu na mwamba wa wokovu wangu.
27 Nami nitamjalia kuwa mzaliwa wangu wa kwanza,Kuwa juu sana kuliko wafalme wa dunia.
28 Hata milele nitamwekea fadhili zangu,Na agano langu litafanyika amini kwake.
29 Wazao wake nao nitawadumisha milele,Na kiti chake cha enzi kama siku za mbingu.
30 Wanawe wakiiacha sheria yangu,Wasiende katika hukumu zangu,
31 Wakizihalifu amri zangu,Wasiyashike maagizo yangu,
32 Basi, nitawarudi makosa yao kwa fimbo,Na uovu wao kwa mapigo.