6 Adui wamekoma na kuachwa ukiwa milele.Nayo miji yao uliing’oa;Hata kumbukumbu lao limepotea.
7 Bali BWANA atakaa milele,Ameweka kiti chake tayari kwa hukumu.
8 Naye atauhukumu ulimwengu kwa haki;Atawaamua watu kwa adili.
9 BWANA atakuwa ngome kwake aliyeonewa,Naam, ngome kwa nyakati za shida.
10 Nao wakujuao jina lako wakutumaini Wewe,Maana Wewe, BWANA hukuwaacha wakutafutao.
11 Mwimbieni BWANA akaaye Sayuni,Yatangazeni kati ya watu matendo yake.
12 Maana mlipiza kisasi cha damu awakumbuka,Hakukisahau kilio cha wanyonge.