6 Mtu mjinga hayatambui hayo,Wala mpumbavu hayafahamu.
7 Wasio haki wakichipuka kama majaniNa wote watendao maovu wakistawi.Ni kwa kusudi waangamizwe milele;
8 Bali Wewe, BWANA, U Mtukufu hata milele.
9 Maana hao adui zako, Ee BWANA,Hao adui zako watapotea,Na watendao maovu watatawanyika wote pia.
10 Bali pembe yangu umeiinua kama pembe ya nyati,Nimepakwa mafuta mabichi.
11 Na jicho langu limewatazama walioniotea,Sikio langu limesikia habari za waovu walionishambulia.
12 Mwenye haki atasitawi kama mtende,Atakua kama mwerezi wa Lebanoni.