7 Nao husema, BWANA haoni;Mungu wa Yakobo hafikiri.
8 Enyi wajinga miongoni mwa watu, fikirini;Enyi wapumbavu, lini mtakapopata akili?
9 Aliyelitia sikio mahali pake asisikie?Aliyelifanya jicho asione?
10 Awaadibuye mataifa asikemee?Amfundishaye mwanadamu asijue?
11 BWANA anajua mawazo ya mwanadamu,Ya kuwa ni ubatili.
12 Ee BWANA, heri mtu yule umwadibuye,Na kumfundisha kwa sheria yako;
13 Upate kumstarehesha siku za mabaya,Hata asiye haki atakapochimbiwa shimo.