1 Njoni, tumwimbie BWANA,Tumfanyie shangwe mwamba wa wokovu wetu.
2 Tuje mbele zake kwa shukrani,Tumfanyie shangwe kwa zaburi.
3 Kwa kuwa BWANA ni Mungu mkuu,Na Mfalme mkuu juu ya miungu yote.
4 Mkononi mwake zimo bonde za dunia,Hata vilele vya milima ni vyake.
5 Bahari ni yake, ndiye aliyeifanya,Na mikono yake iliumba nchi kavu.
6 Njoni, tuabudu, tusujudu,Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.