1 BWANA ametamalaki, nchi na ishangilie,Visiwa vingi na vifurahi.
2 Mawingu na giza vyamzunguka,Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake.
3 Moto hutangulia mbele zake,Nao huwateketeza watesi wake pande zote.
4 Umeme wake uliuangaza ulimwengu,Nchi ikaona ikatetemeka.