2 Mawingu na giza vyamzunguka,Haki na hukumu ndio msingi wa kiti chake.
3 Moto hutangulia mbele zake,Nao huwateketeza watesi wake pande zote.
4 Umeme wake uliuangaza ulimwengu,Nchi ikaona ikatetemeka.
5 Milima iliyeyuka kama nta mbele za BWANA,Mbele za Bwana wa dunia yote.
6 Mbingu zimetangaza haki yake,Na watu wote wameuona utukufu wake.
7 Na waaibishwe wote waabuduo sanamu,Wajivunao kwa vitu visivyofaa;Enyi miungu yote, msujuduni Yeye.
8 Sayuni imesikia na kufurahi,Binti za Yuda walishangilia,Kwa sababu ya hukumu zako, Ee BWANA.