4 Mshangilieni BWANA, nchi yote,Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi.
5 Mwimbieni BWANA zaburi kwa kinubi,Kwa kinubi na sauti ya zaburi.
6 Kwa panda na sauti ya baragumu.Shangilieni mbele za Mfalme, BWANA.
7 Bahari na ivume na vyote viijazavyo,Ulimwengu nao wanaokaa ndani yake.
8 Mito na ipige makofi,Milima na iimbe pamoja kwa furaha.