2 Umejivika nuru kama vazi;Umezitandika mbingu kama pazia;
3 Na kuziweka nguzo za orofa zake majini.Huyafanya mawingu kuwa gari lake,Na kwenda juu ya mabawa ya upepo,
4 Huwafanya malaika zake kuwa pepo,Na watumishi wake kuwa moto wa miali.
5 Uliiweka nchi juu ya misingi yake,Isitikisike milele.
6 Uliifunika kwa vilindi kama kwa vazi,Maji yalikuwa yakisimama juu ya milima.
7 Kwa kukemea kwako yakakimbia,Kwa sauti ya radi yako yakaenda zake kasi,
8 Yakapanda milima, yakatelemka mabondeni,Mpaka mahali ulipoyatengenezea.