4 Uwape sawasawa na vitendo vyao,Na kwa kadiri ya ubaya wa kufanya kwao,Uwape sawasawa na kazi ya mikono yao,Uwalipe stahili zao.
5 Maana hawazifahamu kazi za BWANA,Wala matendo ya mikono yake.Atawavunja wala hatawajenga;
6 Na ahimidiwe BWANA.Maana ameisikia sauti ya dua yangu;
7 BWANA ni nguvu zangu na ngao yangu.Moyo wangu umemtumaini,Nami nimesaidiwa;Basi, moyo wangu unashangilia,Na kwa wimbo wangu nitamshukuru.
8 BWANA ni nguvu za watu wake,Naye ni ngome ya wokovu kwa masihi wake.