1 Heri aliyesamehewa dhambi,Na kusitiriwa makosa yake.
2 Heri BWANA asiyemhesabia upotovu,Ambaye rohoni mwake hamna hila.
3 Niliponyamaza mifupa yangu ilichakaaKwa kuugua kwangu mchana kutwa.
4 Kwa maana mchana na usikuMkono wako ulinilemea.Jasho langu likakauka hata nikawaKama nchi kavu wakati wa kaskazi.
5 Nalikujulisha dhambi yangu,Wala sikuuficha upotovu wangu.Nalisema, Nitayakiri maasi yangu kwa BWANA,Nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.