9 Tumezitafakari fadhili zako, Ee Mungu,Katikati ya hekalu lako.
10 Kama lilivyo jina lako, Ee Mungu,Ndivyo na sifa yako hata miisho ya dunia.Mkono wako wa kuume umejaa haki;
11 Na ufurahi mlima Sayuni.Binti za Yuda na washangilieKwa sababu ya hukumu zako.
12 Tembeeni katika Sayuni,Uzungukeni mji,Ihesabuni minara yake,
13 Tieni moyoni boma zake,Yafikirini majumba yake,Mpate kuwaambia kizazi kitakachokuja.