2 Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu,Nizione nguvu zako na utukufu wako.
3 Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai;Midomo yangu itakusifu.
4 Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai;Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.
5 Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono;Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.
6 Ninapokukumbuka kitandani mwangu,Nakutafakari Wewe makesha yote ya usiku.
7 Maana Wewe umekuwa msaada wangu,Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia.
8 Nafsi yangu inakuandama sana;Mkono wako wa kuume unanitegemeza.