14 Akawaongoza kwa wingu mchana,Na usiku kucha kwa nuru ya moto.
15 Akapasua miamba jangwani;Akawanywesha maji mengi kama maji ya vilindi.
16 Akatokeza na vijito gengeni,Akatelemsha maji kama mito.
17 Lakini wakazidi kumtenda dhambi,Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu.
18 Wakamjaribu Mungu mioyoni mwaoKwa kutaka chakula kwa tamaa zao.
19 Naam, walimwamba Mungu, wakasema,Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?
20 Tazama, aliupiga mwamba;Maji yakabubujika, ikafurika mito.Pia aweza kutupa chakula?Atawaandalia watu wake nyama?