16 Akatokeza na vijito gengeni,Akatelemsha maji kama mito.
17 Lakini wakazidi kumtenda dhambi,Walipomwasi Aliye juu katika nchi ya kiu.
18 Wakamjaribu Mungu mioyoni mwaoKwa kutaka chakula kwa tamaa zao.
19 Naam, walimwamba Mungu, wakasema,Je! Mungu aweza kuandika meza jangwani?
20 Tazama, aliupiga mwamba;Maji yakabubujika, ikafurika mito.Pia aweza kutupa chakula?Atawaandalia watu wake nyama?
21 Hivyo BWANA aliposikia akaghadhibika;Moto ukawashwa juu ya Yakobo,Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.
22 Kwa kuwa hawakumwamini Mungu,Wala hawakuutumainia wokovu wake.