21 Hivyo BWANA aliposikia akaghadhibika;Moto ukawashwa juu ya Yakobo,Hasira nayo ikapanda juu ya Israeli.
22 Kwa kuwa hawakumwamini Mungu,Wala hawakuutumainia wokovu wake.
23 Lakini aliyaamuru mawingu juu;Akaifungua milango ya mbinguni;
24 Akawanyeshea mana ili wale;Akawapa nafaka ya mbinguni.
25 Mwanadamu akala chakula cha mashujaa;Aliwapelekea chakula cha kuwashibisha.
26 Aliuelekeza upepo wa mashariki mbinguni;Akaiongoza kusi kwa uweza wake.
27 Akawanyeshea nyama kama mavumbi,Na ndege wenye mbawa,Kama mchanga wa bahari.