1 Maskani zako zapendeza kama nini,Ee BWANA wa majeshi!
2 Nafsi yangu imezionea shauku nyua za BWANA,Naam, na kuzikondea.Moyo wangu na mwili wanguVinamlilia Mungu aliye hai.
3 Shomoro naye ameona nyumba,Na mbayuwayu amejipatia kioto,Alipoweka makinda yake,Kwenye madhabahu zako, Ee BWANA wa majeshi,Mfalme wangu na Mungu wangu.
4 Heri wakaao nyumbani mwako,Wanakuhimidi daima.