5 Wawagharikisha, huwa kama usingizi,Asubuhi huwa kama majani yameayo.
6 Asubuhi yachipuka na kumea,Jioni yakatika na kukauka.
7 Maana tumetoweshwa kwa hasira yako,Na kwa ghadhabu yako tumefadhaishwa.
8 Umeyaweka maovu yetu mbele zako,Siri zetu katika mwanga wa uso wako.
9 Maana siku zetu zote zimepita katika hasira yako,Tumetowesha miaka yetu kama kite.
10 Siku za miaka yetu ni miaka sabini,Na ikiwa tuna nguvu miaka themanini;Na kiburi chake ni taabu na ubatili,Maana chapita upesi tukatokomea mara.
11 Ni nani aujuaye uweza wa hasira yako?Na ghadhabu yako kama ipasavyo kicho chako?