6 Njoni, tuabudu, tusujudu,Tupige magoti mbele za BWANA aliyetuumba.
7 Kwa maana ndiye Mungu wetu,Na sisi tu watu wa malisho yake,Na kondoo za mkono wake.Ingekuwa heri leo msikie sauti yake!
8 Msifanye migumu mioyo yenu;Kama vile huko MeribaKama siku ya Masa jangwani.
9 Hapo waliponijaribu baba zenu,Wakanipima, wakayaona matendo yangu.
10 Miaka arobaini nalihuzunika na kizazi kile,Nikasema, Hao ni watu waliopotoka mioyo,Hawakuzijua njia zangu.