4 Neno Moja nimelitaka kwa BWANA,Nalo ndilo nitakalolitafuta,Nikae nyumbani mwa BWANASiku zote za maisha yangu,Niutazame uzuri wa BWANA,Na kutafakari hekaluni mwake.
5 Mradi atanisitiri bandani mwake siku ya mabaya,Atanisitiri katika sitara ya hema yake,Na kuniinua juu ya mwamba.
6 Na sasa kichwa changu kitainukaJuu ya adui zangu wanaonizunguka.Nami nitatoa dhabihu za shangwe hemani mwake;Nitaimba, naam, nitamhimidi BWANA.
7 Ee BWANA, usikie, kwa sauti yangu ninalia,Unifadhili, unijibu.
8 Uliposema, Nitafuteni uso wangu,Moyo wangu umekuambia,BWANA, uso wako nitautafuta.
9 Usinifiche uso wako,Usijiepushe na mtumishi wako kwa hasira.Umekuwa msaada wangu, usinitupe,Wala usiniache, Ee Mungu wa wokovu wangu.
10 Baba yangu na mama yangu wameniacha,Bali BWANA atanikaribisha kwake.