1 Unirehemu, Ee Mungu, unirehemu mimi,Maana nafsi yangu imekukimbilia Wewe.Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako,Hata misiba hii itakapopita.
2 Nitamwita MUNGU Aliye juu,Mungu anitimiziaye mambo yangu.
3 Atapeleka toka mbinguni na kuniokoa,Atukanapo yule atakaye kunimeza.Mungu atazipelekaFadhili zake na kweli yake
4 Nafsi yangu i kati ya simba,Nitastarehe kati yao waliowaka moto.Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale,Na ndimi zao ni upanga mkali.